May 29, 2007 09:46 PM PDT
Serikali imetoa tamko lake na inaendelea kushikilia uzi ule ule wa kutowatambua vijana wetu waliokwama Ukraine. Hata hivyo, wakati umefika wa kuwasaidia vijana hawa kupitia akaunti iliyofunguliwa ili waendelee kusoma na si kurudishwa nyumbani wakiwa wameshindwa. Nimejibu hoja za serikali zilizotolewa jumatatu ambazo kwa kile zimeonesha hawakufuatilia suala hili kabisa na wamekurupuka tu kujibu kwa kusoma habari magazetini! Ili kuchangia hawa vijana tafadhali fuata maelekezo kama yanavyopatikana kwenye www.jamboforums.com au bonyeza hapa kupata nakala ya akaunti za benki.
Michangokwawanafunziukraine
Pichani ni wanafunzi siku ya kwanza walipowasiri nje ya ubalozi wa Uingereza jijini Kiev, huko Ukraine.