Player_logo Podcasts Community Create a Podcast
powered by podOmatic
460>_1805073

Ni mgongano wa kihistoria ambao ulipaswa kutokea. Ni mgongano ambao hutokea mahali popote panapokuwa na tofauti kubwa kati ya watawala na watawaliwa. Ndivyo ilivyokuwa kwenye Mapinduzi ya Ufaransa, Mapinduzi ya Marekani na Mapinduzi ya Bolshevik (Urusi).

Ni yale yale yaliyotokea na kusababisha mapinduzi ya Cuba yaliyomuingiza Castro madarakani. Ndiyo! Ni yale yale yaliyotokea pia kwenye mapinduzi ya Zanzibar!

Migongano ya namna hiyo asili yake mara zote ni pale wananchi wanapotambua kuwa hawana usawa na watawala wao na ya kuwa tofauti ya maisha yao na yale ya watawala ni kubwa mno na ya kwamba mwananchi wa kawaida anajikuta hana nafasi yoyote aidha ya kufanikiwa au ya kuweza kuishi maisha yenye utu, usawa, haki na heshima.

Nchi chache zimeweza kupitia mgongano huo kwa njia ya nguvu (kama mifano niliyotoa) au kama ilivyotokea huko Ukraine na Georgia miaka ya karibuni kwa njia ya nguvu ya umma.

Tanzania yetu inapitia mgongano huo katika hatua zake za awali. Silaha ambayo wananchi wanatumia leo hii ni nguvu yao ya hoja na wanatarajiwa kubadilisha serikali yao kwa nguvu ya kura.

Hata hivyo hilo halitakuwa rahisi kwani dalili yote inaonesha kuwa watawala hawako laini kuruhusu mabadiliko makubwa ya kiutawala yenye kupendelea wananchi wa kawaida. Hivyo, mgongano unaendelea. Swali ni nani ashinde? Na ni nani ataamua mshindi!?

Nisikilize:

[PLAY]
460>_1786550

Kwa namna fulani tunaamini kuwa sisi tuna upendeleo wa aina fulani kwa Mwenyezi Mungu, kwamba nchi yetu kwa sababu upendeleo wa pekee basi haitapata majanga. Hatujajifunza kwa ajali zinazotea mara kwa mara za mabasi, hatujajifunza kwenye ajali za majini, hatujajifunza kwenye milipuko ya mabomu na kwa hakika tuko kama tumepigwa ganzi ya aina fulani hivi.

Pamoja na kutoa pole na rambirambi, ni lazima tujiulize tutaendelea mpaka kulini kwa kutegemea rehema za Mungu? Sitoshangaa leo tutaambiwa katika Hotuba ya Rais kuwa haya yalikuwa ni mapenzi ya Mungu na ya kuwa wanaunda tume kuchunguza kitu gani kilisababisha na wananchi wasiwe na wasiwasi hali ni shwari na halikuwa tukio la kighaidi..

Katika wazimu wetu tutasema Amen.. na kusahau kabisa mlolongo wa kutojiandaa na majanga ambao serikali ya CCM imeuendeleza kwa miaka kadhaa sasa na kutuacha tuishi kwa bahati!

Jana, tumeikwepa risasi! Huko mbeleni (na itakuwa hivyo kwani majanga yataendelea kutokea hata kama tunaombea yasitokee, ndiyo kanuni ya ulimwengu!) tutakuja kulia kama tulivyolia kwenye MV. Bukoba na Bahi! (wengine wanajiuliza "Bahi?"! wameshasahau!

[PLAY]
460>_1766968
Salaam, Suala la DECI ni marudio tu ya michezo mingine kama hiyo ambayo imeshawahi kutokea huko nyuma. Jinsi suala la DECI lilivyoshughulikiwa linaonesha ni wazi hakuna utaratibu mzuri wa kushughulikia michezo hii na inakuwa kama tunaanza moja. Hatuelewi ni kwanini michezo hii inarudiwa rudiwa hadi inafikia inapofikia ndio kama watu waliokurupushwa watendaji wa serikali ndio wanaanza kufanya kazi. Twende na tuwe cheche!
460>_1750188
Salaam, Pamoja na habari mwanana za wiki hii ambazo zitagusa fikra zako na maoni ya kuthubutu ambayo huwezi kuyapata mahali pengine popote tunakuletea pia habari zinazoendelea kila wakati. Kwa kupata email ya habari mpya na kupokea kijarida chetu cha "Cheche" kwa kutumia barua pepe tuandikie kwenye anuani ya mhariri iliyoko kwenye kijarida. Kuna habari mbili kubwa ambazo zimeanza kusikika saa hii: a. Wakuu wa Mikoa wapanguliwa na kubadilishana vituo mbalimbali, hii inaonesha kugusa mikoa ya Tanga, Dar, Iringa, Kilimanjaro, Dodoma n.k Kimsingi siyo habari kubwa inayostahili kwani kilichofanyika ni kubadilishana ofisi tu. Aliyeshindwa eneo moja kumpeleka jingine hakuondoi tatizo ambalo ni yeye! Baadhi ya mabadiliko hayo: Dr. Ishengoma toka Pwani kwenda Ruvuma Bi. Hajjat Amina Said toka Iringa kwenda Pwani Bw. Abdulazziz toka Tanga kwenda Iringa Bi. Monica Mbega toka Ruvuma kwenda Kilimanjaro (huyu ni yule Mkuu wa Mkoa wa "Kamtumbwi ka Kikwete") tunaendelea kufuatilia kujua wa Kilimanjaro ameenda wapi na kama Mbeya wamebadilishiwa (maana na siasa zao huko ni vurugu kuwa na Mkuu wa Mkoa ambaye ni mwenyeji wa huko!) b. Kuna habari kuwa ofisi za DECI zimefungwa au DECI yenyewe imesimamishwa. Utaona katika toleo letu la leo tulitoa wito huo kwani kuiacha kuendelea kufanya kazi katika mazingira ya sasa ni kulea uovu. Kwa hiyo tunasubiri tuone mwitikio utakuwaje kwani tangu makala zetu mbili (iliyotoka kwenye Cheche wiki iliyopita) na iliyotoka leo kwenye Mwanahalisi kuna watu wamechukizwa na wengine wameapa kufanya vitu vibaya endapo DECI itafungwa. Tunatumaini vikosi vyetu vya usalama viko tayari kusimamia haki. Na hii ni habari ndogo c. Kwa wakazi wa mikoa ya kanda ya Ziwa, wiki hii wataanza kuona gazeti jipya la habari na maoni na tunarajia kuwa na makala za Mwanakijiji humo pia. Kaeni chonjo. Basi na sisi na twende na tuwe "Cheche"! Jipatie nakala ya cheche: http://www.forums.mwanakijiji.com/showthread.php?t=729
460>_1655326
Salaam, Tumepata nafasi ya kuzungumza kwa kirefu na Mhe. Lucas Selelii Mbunge wa Nzega, miongoni mwa wabunge wenye msimamo wa kimabadiliko na miongoni mwa vinara wa vita dhidi ya ufisadi ndani ya CCM na katika Taifa. Tafadhali hakikisha unasoma sehemu ya ahadi yetu kwani tuna ujumbe muhimu kwa wasomaji wetu na wanachama wetu. Ungana nasi pia kwenye mijadala motomoto kwenye forum yetu ya http://www.mwanakijiji.com ambapo mojawapo ya mijadala ya kina ni suala la Rais wa zamani Mzee Ally Hassan Mwinyi kushambuliwa siku ya jana kwenye maadhimisho ya Siku Kuu ya Maulidi pale ukumbi wa Diamond Jubilee. Tushirikishe mawazo yako. Vivyo ni mahali ambapo kila tunapopata habari unakuwa wa kwanza kabla hujazisoma habari hizo kwenye magazeti, kusikia radioni au kutazama kwenye luninga. Karibu! Twende na tuwe Cheche!
[PLAY]
460>_1632441

Mpango wa serikali kutaka kuyanunua majenereta ya kuzalisha umeme ambayo yaliletwa nchini na Kampuni ya Dowans katika mkataba wake na kampuni feki iliyoumbuliwa ya Richmond hautokani na kulazimika kufanya hivyo bali hali halisi ya hali ya nishati nchini ndiyo inalazimisha serikali kupanga kuchukua hatua hiyo. Hayo yamesemwa na Waziri wa Nishati na Madini Mhe. William Ngeleja alipozungumza na tovuti hii hapo jana kuelezea kile ambacho kinaonekana mgongano wa kimtazamo kati ya Wizara, kamati mbili za Bunge na hisia za makundi ya Watanzania.

Akizungumza nasi kwa kirefu Mhe. Ngeleja amejenga hoja kuwa suala la ununuzi wa mitambo hiyo halihusiani na masuala ya kifisadi kama wengi wanavyohisi huku yeye mwenyewe akisema kuwa "siyo wote mafisadi". Bw. Ngeleja alitumua muda mrefu kushawishi kuwa mpango huu ni mzuri kwa maslahi ya Taifa na kuna kila sababu ya kuangalia kwa ukaribu na kuubali.

Ni kwa kiasi gani ameweza au anaweza kushawishi uamuzi ni wawasikilizaji wetu wenyewe. Unaweza kusikiliza mahojiano hayo kwenye tovuti yetu hii au kwa kusikiliza kupitia tovuti yetu ya http:/www.mwanakijiji.podomatic.com ambapo unaweza kuyapata mahojiano hayo kwenye Itunes au Ipod yako. Sikiliza wewe mwenyewe kama Mhe. Ngeleja amejenga hoja ya kukushawishi kukubali serikali inunue mtambo huu au ungependa serikali isiendelee nao.

Sisi katika tovuti yetu tutatoa msimamo wetu kwenye kijarida cha Cheche kitakachotoka hapo kesho.

[PLAY]
460>_1626774
[IMG]http://www.mwanakijiji.com/images/stories/habari/gallery/taarifa2008.jpg[/IMG] Leo Machi 1, 2009 ni miaka mitatu tangu tuanze kuandika kama wanaharakati na kuanza matangazo yetu yenye kujenga hoja mbalimbali. Ni miaka mitatu ambayo imetimia ndani yetu moto wa mwamko mpya ukizidi kuwaka na kuchochewa kila siku kama tanuru ya chuma! Katika kuangalia mwaka uliopita na kutazama mwaka huu mpya tumeandaa ripoti yetu hii ya shughuli zetu kama tulivyofanya mwaka jana. Kwa mara ya kwanza tumeenda mbele zaidi kwa kuweka mambo mengi wazi ambayo tunaamini kwa wale mashabiki, wanachama na wanaotuunga mkono kuweza kufahamu. Tunatumaini taarifa hii ni kile kidogo tunachofanya katika kuwajibika mbele zenu. Kwa unyenyekevu mkubwa naomba kuwasilisha. Hii nayo iwe ushuhuda! M.M. Mwanakijiji Bonyeza Hapa: [url]http://www.box.net/shared/fx8bd7oxi7[/url]
460>_1603912
Natamani ningeweza kusema kwa nguvu ninachosema kisema hapa. Natamani ningekuwa na sauti kubwa zaidi kuweza kusikika kuhusu mauaji ya Leticia Bahati siku tatu zilizopita. Ninachojiuliza ni kwanini Masha bado ni Waziri wa Mambo ya Ndani? Lakini kuna maswali makubwa zaidi ya hilo ambayo ninayauliza leo kwenye "Nguvu ya Hoja"! Sikiliza.
[PLAY]
460>_1561069
Salaam enyi wana mapambano ya fikra,

Toleo letu kama tulivyotaarifa lilichelewa kutoka hadi leo hii. Ndani yake kuna habari nyeti na nzito na pia kuna makala ya kusisimua yenye mikwara kutoka kwa Dr. Wilbroad Slaa. Zaidi ya yote huwezi kukosa maoni ya kishujaa ya Jessica. Pia hoja kuhusu miaka 32 ya CCM inatolewa kwa nguvu zote.

Ni matumaini yetu kwa namna fulani tumeweza na tunaendelea kuweza kushiriki katika mijadala mbalimbali ya kitaifa na tunakukurabisha uungane nasi kwenye baraza la mijadala kwenye http://www.mwanakijiji.com.

Wakati huo huo utaona kuwa tumeongeza sehemu ya kuweka picha mbalimbali kwenye tovuti yetu na unaweza kufungua albam yako ya picha mbalimbali ukizingatia taratibu na kanuni zetu.

Na wewe nenda, ukawe Cheche! Mhariri Pata nakala yako ya bure hapa: http://www.mwanakijiji.com

460>_1548349

Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda ametumia nafasi yake ya kujibu maswali Bungeni kugusa hisia za wabunge kwa kuonesha uchungu uliomgusa kufuatia mauaji ya maalbino ambayo yamekuwa yakiendelea nchini.

WM Pinda alimwaga machozi hayo baada ya kuulizwa kuhusu kufafanua kauli yake iliyotaka watu watakaoshukiwa au kutuhumiwa mauaji ya albino na wao kuuawa hapo hapo. Alipoulizwa kwanini ahalalishe mauaji hayo na kwanini atoe kauli zinazonesha kukikanzina na utawala wa sheria na Katiba ambao ni msingi wa TAifa letu, Mhe. Pinda alielezea kwa kirefu juu ya safari yake na yale aliyoyaona na kuelezea kuwa mtu yeyote akiyaona aliyoyaona hana sababu tena ya kufuata sheria bali kuchukua hatua mikononi.

Alielezea kauli yake kuwa ni ya kutishia watuhumiwa hao kuwa wajue serikali iko fed up na mauaji ya Albino. Hata hivyo hakuifuta kauli hiyo wala kusema kwamba watuhumiwa wote wafikishwe kwenye vyombo vya sheria au kuwataka wananchi kuhakikisha katika kupambana na mauaji haya wao wenyewe hawajikuti wakivunja sheria za nchi.

Swali ambalo linaonekana kuwagawa wananchi ni je kutokana na mauaji haya ya albino ipo haja ya wananchi kufuata sheria au wakimkuta mtu wanayemdhania kuwa ndiye muhusika wamchukulie hatua mikononi kama inavyofanywa kwa vibaka, wezi wa kuku na watuhumiwa wengine ambao mara nyingi hupata kibano papo kwa hapo?

Msikilize Pinda akikwepa kujibu swali aliloulizwa.

[PLAY]

Previous Page  |  Next Page