Player_logo Podcasts Community Create a Podcast
716454322
460>_995931

Tulikokuwa tunaenda siko, tumeamua kugeuka" - hayo ni baadhi ya maneno ya Mhe. Anne Kilango Malecela akizungumza na KLH News siku chache zilizopita akielezea mabadiliko ya wabunge wa CCM linapokuja suala la kulinda maslahi ya Taifa.

Kati ya mambo ambayo anayazungumzia ni pamoja na hali ya kisiasa nchini, kifo cha Ballali, kwanini wabunge wa CCM walikuwa wanaitetea serikali yao hata ilipokuwa inaharibu, kwanini anaamini Kikwete ni kweli anataka mabadiliko na masuala mengine kemkem.

Mahojiano yangu hayo na Mhe. Anne Kilango Malecela (CCM - Same Mashariki) yatarushwa siku ya Ijumaa kupitia KLH News International na pia tunatarajia yataweza kusomwa kwenye mojawapo ya magazeti ambayo yamekubali kutupa nafasi.

Mimi niko impressed na watu mara chache sana.. this is one of those times

[PLAY]
460>_985328
Hii ni marudio ya show tuliyofanya siku ya Jumapili. NI sehemu tu ya onesho hilo.
[PLAY]
460>_979164

What happened? why did it happen? do you have any idea who did it and why? do you believe it. What next!?

KLHN will air a Live Show on Sunday at 2:00PM EST (1:00PM CST, 9:00PM East African Time) to discuss the events that have transpired this past week especially the death that is shrouded in mystery and speculation of former Bank of Tanzania Dr. Daudi Thomas Said Ballali who passed away last Friday.

You can participate in the "live" show through a phone call in at 1 248 686 2010 during the live show, or you can call the same line through out Saturday and live your short message of your thoughts about the death and the events surrounding his passing.

Otherwise you can also write an email of not more than six lines paragraph to express your thought/s (anything more than that will be deleted) on the matter. Write to klhnews(at)klhnews.com

You can hear the show through http://www.bongoradio.com

Exclusive with this show is a suprise guest; an outspoken member of Parliament through CCM and a few other MPs from the ruling party and the opposition who will respond to the question posed to them on whether the death of Gov. Ballali should impact in anyway,shape or form the ongoing EPA investigation and how they received the news of his death.

This event is brought to you in association with JamiiForums and Bongo Radio.

NB: I know people can type and scream behind their computers and show their anger through the speed of their fingers.. it is about time to be heard.. let us hear that anger, frustrations, concerns etc.. don't be scared that they might know who you are.. it is about time to be heard, I know I will...

NOTICE: Any Tanzania Radio Station or media House that would like to stream or air this "live" show you are most welcome to do so just let us know so that we can acknowledge your listeners and identify your station.

DARING TO BOLDY GO, WHERE NO ONE ELSE DARE TO!

460>_930306
Aliyewahi kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Dr. Daud Balali amefariki dunia. Habari ambazo zimeanza kusikika tangu jana jioni na kuthibitishwa na ndugu zake zimesema kuwa Gavana Balali amefariki mwishoni mwa juma na mipango ya mazishi inafanywa. Anatarajiwa kuzikwa huko huko Marekani. Inatarajiwa taarifa ya kifo chake kutangazwa Tanzania baadaye leo. Sikiliza matangazo kuhusu kifo hicho hapa au kwa kutwa nzima ya kesho tutakuwa tunaleta maendeleo yoyote ya habari hii kwenye tovuti yetu ya http://www.klhnews.com ambako "we bring the news first".
[PLAY]
460>_909826

Karibu wiki moja iliyopita Mhe. Zitto Kabwe alizungumza na jumuiya ya Watanzania waishio Jimbo la Michigan nchini Marekani. Mazungumzo hayo yaliyofanyika wakati wa hafla ya chakula cha jioni aliyoandaliwa Bw. Zitto yaligusia mambo mbalimbali na hasa kuwataarifu wanajumuiya hiyo mambo mbalimbali yanayoendelea nyumbani na pia kusikiliza maoni na maswali yao.

Matangazo ya leo basi ni hotuba ya Mhe. Zitto kwa jumuiya hiyo na sehemu ya maswali na majibu, yote ni uncut and an edited. Makosa mengine yoyote ya kurekodi hasa mwanzoni kidogo ni ya KLHN.

Pichani Mhe. ZItto akijiandaa kuzungumza na wanajumuiya ya TAMI - Tanzanians Association of Michigan. Huko Detroit eneo la Maili Nane.

[PLAY]
460>_900839

Gavana wa Benki Kuu, Dk Beno Ndullu (katikati) akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja wa Benki ya Maendeleo Afrika Mashariki (EADB), Andulile Mwakalyelye (kulia) alipotembelea mabanda wakati wa mkutano wa Makandarasi na Taasisi za fedha kwenye viwanja vya Karimjee Dar es Salaam. Kushoto ni Msajili wa Bodi ya Makandarasi, Mhandisi Boniface Muhegi

Kuna mahali katika serikali yetu watu hawawasiliani. Nina kila sababu ya kuamini kuwa kuna mtu ambaye hafikishi habari kwa mwingine kiasi kwamba tumefikia mahali watumishi wa wizara ile ile na ambao kimsingi wanatakiwa kuwasiliana inaonekana hawawasiliani.

Hebu fikiria, Katibu Mkuu wa Hazina anasimama na kutetea maamuzi yake kuwa alipotia sahihi kwenye kampuni ya Tangold kama mmoja wa wakurugenzi alijua kuwa kampuni hiyo ni mali ya serikali. Siyo hivyo tu aliyekuwa Waziri wa Fedha Bi. Zakhia Meghji aliliambia Bunge kuwa kampuni hiyo iliyochukua nafasi ya kampuni nyingine ya "serikali" ya Meremeta ni mali ya serikali.

Kabla hilo halijatulia Gavana wa Benki Kuu ambayo kampuni hiyo ilimegewa karibu Bilioni 155 kwa vile ni kampuni ya serikali anaibuka kesho yake na kusema kuwa watu wasiihusishe Benki hiyo Kuu na Kampuni hiyo kwani hakuna ushahidi wowote kuwa kampuni hiyo inamilikiwa na serikali

Sasa nani anaweza kuwa na uwezo wa kujua juu ya Kampuni hii kati ya Katibu Mkuu Hazina ambaye ni Mkurugenzi wa Tangold na Gavana wa Benki Kuu iliyotoa mabilioni kwa taasisi hiyo?

Hivi Watanzania tumekosa nini hadi tuburuzwe kama watoto wanaochezewa mchezo wa Karata tatu? Hivi mtu akimuuliza Kikwete kama Kampuni ya Tangold ni ya serikali atakuwa na jibu kweli wakati Hazina na Benki Kuu hawakubaliani?

Hili nalo linanikumbusha juu ya Mgodi wa Buhemba ambao tuliambiwa kuwa ni mali ya serikali lakini Mkaguzi Mkuu wa serikali anasema hana jina hilo katika orodha ya makampuni ya serikali. Sasa mgodi huo unalindwa na Polisi, nani anaumiliki?

Kuna mtu yeyote anaweza kutoa jibu? Hivi kweli tumefikia mahali hatujui hata nani anamiliki mgodi mkubwa kama Buhemba? Hivi tukiuliza nani anamiliki Ikulu yetu tunaweza kuwa tunatafuta ugomvi? Tukisema kuna mafisadi hivi kweli watakuwa na sababu ya kututafuta? Au tuanze kampeni kwa kupitia wahisani dhidi ya misaada au tutaambiwa tunataka watu wa kawaida wapate shida? Ni nini kitatufanya tuchore mstari?

Naomba nitoe wito kwa Waziri wetu wa Fedha atuambie bila kujiuma uma, ni nani anamiliki Tangold na Buhemba? is this too much to ask as citizens of our beloved country au ndio imekuwa ni mradi wa Usalama wa Taifa?

460>_883707

Mbunge wa Igunga Mhe. Rostam Aziz (CCM) ameamua kulishtaki gazeti la Mwanahalisi na wakati huo huo kulitishia gazeti la Raia Mwema kuwa atalifungulia mashtaka endapo halitaomba radhi kwa mojawapo ya makala zake.

Bw. Rostam anakuwa kiongozi wa kwanza ambaye amekuwa akitajwa na vyombo vya habari kuhusu ufisadi aliyeamua kwenda mahakamani. Kwa namna ya pekee hli linaashiria mambo kadhaa.

Kwanza, endapo mahakama itaridhia maombi yake basi masuala ya Richmond na Rostam yanaweza yasitajwe kwenye sentensi moja kwani kesi itakuwa mahakamani . Huu ni mchakato wa Kisheria na vyombo husika vitatakiwa kuheshimu, ingawa hilo halitufungi sisi wengine kutolea maoni

Pili, kujaribu kunyamazisha vyombo hivyo vya habari endapo kutakubaliwa na mahakama basi kutazuia habari mpya kuweza kuchapwa na gazeti hilo . Hata hivyo, sisi wengine tutaweza kuendelea kutolea maoni

Jambo la tatu ni kuwa Bw. Rostam amefanya jambo la maana kwa kuamua kwenda mahakamani hasa kwa vile anaamini haki yake inatishiwa na jina lake kuchafuliwa. Hivyo, uamuzi wake ni mfano wa kuigwa kwa wengine ambao wanahisi kuonewa au kutotendewa haki ili watumie vyombo vya sheria kutafuta haki hiyo badala ya kukimbilia kwenye TV au radio kujisafisha.

Hata hivyo, kama kesi hii itanedelea au itaishia pembeni hatuna uhakika. Hata hivyo vyanzo vyangu vya karibu na MwanaHalisi vimenihakikishia kuwa hawana mpango wa ku "back down" na wanaendelea kufanyia kazi taarifa nyngine kuhusu Rostam na Richmond. Sisi wengine yetu ni macho tu.

Je wadaiwa wengine na wale wanaotajwa kwenye tuhuma za ufisadi na wenyewe waende mahakamani? Je ndiyo njia pekee ya wao kujisafisha? Kwanini wale wengine waliotishia kwenda mahakamani hawakwenda?

460>_875785
Kwa karibu wiki mbili sasa nimekuwa nikitengeneza hoja na kumulika kama vile kurunzi idara ya Usalama wa Taifa. Sikiliza introduction ya makala yangu maalum kwenye gazeti la "Kulikoni" leo. Kwa wale ambao hampo nyumbani makala hii itawekwa baadaye mchana wa Ijumaa (saa za Marekani) kwenye http://www.klhnews.com upande wa editorial.
[PLAY]
460>_874058

Ndugu zangu, kuna uwezekano mkubwa kwamba itakapofika kiangazi mwaka huu, Taifa letu linaweza kujikuta kwenye upungufu mkubwa wa chakula ambao siyo tu unatishia maisha ya watu wetu bali pia unashusha hadhi na utu wa mwanadamu. Hakuna kitu kinachomdhalilisha mwanadamu na kuweza kumfanya awe mtu kama njaa.

Ni njaa ndiyo inayoweza kumfanya mtu aukane urithi wake wa kwanza kama alivyofanya Esau na ni njaa ambayo ilikuwa inatumika tangu enzi za kale kama silaha ya mwisho ya vita ambayo inalazimisha watu kusalimu amri.

Tanzania tutakabiliwa na njaa ambayo chanzo chake si ukame. Mara nyingi (kama siyo zote) njaa husababishwa na ukame na vita. Hata hivyo njaa ambayo naweza kuiangalia toka mbali na inayosogelea kama simba anyatiaye haitokani na mambo hayo bali makubwa mawili.

a. Kupanda kwa bei ya chakula duniani.
Habari za leo ni kuwa bei ya chakula duniani imepanda kwa haraka kuliko wakati wowote ule na hivyo kusababisha ugumu wa kupatikana kwa chakula. Yaliyotokea Haiti na Misri siku chache zilizopita ni dalili ya ubaya wa hali hiyo. Kwa wale walioko Dar au maeneo yenye masoko ya kudumu na kwenye mialo mbalimbali kanda ya ziwa wanaweza kutusaidia kutuambia kama kumeanza kutokea mabadiliko yanayoonekana ya bei ya chakula siku hizi chache zilizopita.

b. Mvua ya masika.
Hata hivyo naamini kwa upande wa Tanzania kitakachosababisha njaa sana ni hii mvua ambayo imeharibu mashamba na mazao ya watu kiasi kwamba baadhi ya maeneo ambayo kwa kawaida yana chakula cha kutosha yanaweza kujikuta yanahamia mwaka huu. Kama mpunga wa Kyela utakuwa umeathirika kama Dr. Mwakyembe alivyosema kwenye mahojiano yake nami kuna uwezekano kuwa Mwaka huu bei ya Mchele nayo itapanda na hivyo kufanya nafaka hiyo ianze kuwa adimu na kupatikana kwa wachache.

Maeneo ambayo mchele ndiyo chakula kikuu na pia zao la biashara watajikuta wanakabiliwa na upungufu wa fedha za kununulia hata vitu vingine na hivyo kusubiri chakula cha misaada.

Kwa vile tunajua haya yote na ziada; tufanye nini ili tujiandae na njaa ijayo?

460>_872267

Hadi gazeti la Guardian litutangazie kuwa Waziri wetu ameficha Bilioni kisiwani Jersey (thanks Yebox2) wao kina RO walikuwa wapi?

Hadi Kamati Teule ilipotuambia rasmi kuwa RDC ni kampuni hewa RO na timu yake walikuwa wapi?

Niendelee kuorodhesha ushahidi wa uzembe uliokithiri na uvivu wa kufikiri wa taasisi nyeti ya Usalama wa Taifa? Kama wameshindwa kugundua matukio ya economic sabotage yanayoendelea nchini wana faida gani? Hii ya kusafiri na Rais na kutumia vi ear pieces na makoti marefu kama vile wao Secret Service?

Kwanini basi Mkurugenzi wa Idara hiyo Bw. Rashid Othman (Pichani) asijiuzulu kwa ajili ya Usalama wa Taifa!!!

Lakini kabla yake Bw. Cornel Apson Mwang'onda na yeye alishikiri vipi katika kuzembea kulilinda Taifa letu na ni nani mwenye ujasiri wa kumuita na kumhoji?

Isije kuwa Usalama wa haki ya kula na kutanua na fedha za walipa kodi wa Tanzania lakini inapokuja katika kuelezea walifanya nini na pesa hizo inakuwa mbinde?

yes I said it!

Previous Page  |  Next Page